Urasimishaji wa Ujuzi (RPL)UtanguliziUrasimishaji wa Ujuzi Uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi wa Mafunzo (RPL) ni mchakato wa kutambua kutathmini na kuthibitisha ujuzi wa mtu bila kujali jinsi alivyopata ujuzi, lini na kwa muda gani na wapi ujifunzaji umefanyika. Hatua za uthibitishaji wa ujuzi na utunuku wa cheti kwa mwanagenzi (Fundi aliyejifunzia mahali pa kazi pasipo kupita kwenye mfumo rasmi wa mafunzo) hufanywa kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa vya moduli na sifa kamili za Miongozo ya utoaji na tathminini ya Elimu ya Ufundi Stadi. Kwa kuzingatia hili, Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) huandaa na kutoa miongozo ya tathmini kwa moduli zinazotambulika Kitaifa. Walengwa Wa ProgramuWalengwa wa Programu hii ya RPL ni mafundi wenye ujuzi uliopatikana kupitia mafunzo yasiyo rasmi na ujuzi uliopatikana kupitia uzoefu wa maisha au kazi. Mwombaji wa programu ya RPL anaweza kutoka katika sekta rasmi ya uchumi au katika sekta isiyo rasmi. Manufaa Ya Kurasimisha Ujuzi Kupitia Programu Ya RPLProgramu ya Urasimishaji wa Ujuzi Uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi wa Mafunzo (RPL) inamuwezesha fundi aliyejifunza nje ya mfumo rasmi wa mafunzo kuwa na sifa inayotambulika kitaifa na inayoaminika kwa waajiri na sekta mbalimbali ikiwemo Elimu na taasisi za kifedha. Hivyo huleta manufaa mengi, ikiwa ni pamoja na:
Sifa Gani Unapaswa Kuwa Nazo Ili Uweze Kurasmisha Ujuzi Kupitia Programu Ya RPL?
Orodha Ya Fani Unazoweza Kurasimisha Ujuzi Wako Kupitia Programu Ya RPL Kwa SasaKwa sasa waombaji wanaoweza kurasimisha ujuzi kupitia Programu ya RPL wanapaswa kutoka katika fani zifuatazo:
VETA inatarajio kuongeza orodha ya fani kulingana na mahitaji. Mwombaji mwenye ujuzi zaidi ya fani moja anapaswa kuchagua fani moja kwa wakati. Hatua Za Kufuata Ili Kurasimisha Ujuzi WakoIkiwa mwombaji anakidhi vigezo vilivyotajwa hapo juu ataendelea na hatua za uombaji kama ifuatavyo:
VETA inatarajio kuongeza orodha ya fani kulingana na mahitaji. Mwombaji mwenye ujuzi zaidi ya fani moja anapaswa kuchagua fani moja kwa wakati. Mafanikio
|