Karibu

Tathmini Inayozingatia Umahiri (CBA)

Utangulizi

Tathmini Inayozingatia Umahiri (CBA) imeundwa kwa kuzingatia vigezo vilivyobainishwa wazi vya utendakazi ambavyo huweka wazi kabisa kile ambacho mwanafunzi anatarajiwa kuweza kufanya. Ili kufaulu kozi inayozingatia uwezo, mwanafunzi lazima aonyeshe ufaulu wa vigezo vyote vya utendaji ambavyo vinahusishwa na umahiri. Kwa sababu tathmini inayozingatia umahiri (CBA) inahusishwa kwa karibu zaidi na uwezeshaji halisi na mchakato wa kujifunza, kwa hiyo tathmini endelevu na tathmini ya mwisho hutumiwa kumpima mwanafunzi.

Miongozo imezingatia aina kuu mbili za tathmini yaani tathmini endelevu na tathmini ya mwisho. Tathmini zote mbili zinachukuliwa kuwa tathmini muhimu huchukuliwa kama michakato muhimu ya tathmini katika kubainisha mafanikio ya wanafunzi na watahiniwa katika umahiri. Zaidi ya hayo, miongozo inaainisha vigezo vya utunuku wa vyeti na maelezo ya madaraja jinsi yanavyopaswa kuonekana katika cheti cha umahiri.

Miongozo ina sehemu tatu, ambazo zinaakisi makundi makuu mawili ya wanafunzi wanaohitaji Tathmini inayozingatia Umahiri. Miongozo inajumuisha wanafunzi walio katika vyuo vya mafunzo na wanagenzi katika sehemu rasmi za kazi na zisizo rasmi.

Kama njia za tathmini zinayozingatia umahiri katika kutathmini ujuzi, maarifa na mtazamo wa watahiniwa kama zilivyofundishwa wakati wa mafunzo. Kinyume na njia nyingine za tathmini, tathmini inayozingatia umahiri kwa kiasi kikubwa ni mbinu ya tathmini inayomhusu mwanafunzi ambaye anahusishwa moja kwa moja katika michakato yote ya tathmini. Tathmini inayozingatia umahiri inaweza kugawanywa katika aina mbili pana ambazo ni Tathmini Endelevu na Tathmini ya mwisho.

Utaratibu wa Kujiunga na Kozi za Muda Mrefu Kwenye Vyuo vya Veta

VETA imeweka utaratibu na sifa za kujiunga na kozi za muda mrefu kama ifuatavyo:

Nafasi za kujiunga na masomo hutangazwa mwezi wa Agosti kila mwaka. Matangazo hutolewa katika vyombo vya habari nchini pamoja na kwenye tovuti ya VETA yaani www.veta.go.tz

  1. Mwombaji ni lazima awe amemaliza elimu ya msingi, sekondari na kuendelea;

  2. Mwombaji huchukua fomu katika chuo chochote kilichopo karibu. Fomu hizo zina taarifa ya vyuo vyote vinavyomilikiwa na VETA, ikiwa ni pamoja na fani zinazofundishwa na mahali chuo kilipo na kama ni kutwa au bweni;

  3. Mwombaji anaruhusiwa kufanya mtihani wa kujiunga mkoa aliochukua fomu lakini anaweza kuchagua kusoma mkoa wowote anaochagua kulingana na mahitaji yake;

  4. Mwombaji anatakiwa kufanya mtihani wa kujiunga (Aptitude Test) mwezi Oktoba na wale wanaofanikiwa kuchaguliwa hupewa taarifa mwezi Desemba ili kuanza masomo mwezi Januari mwaka unaofuata;

  5. Mwombaji anayefanikiwa hupewa barua ya kujiunga inayofafanua mahitaji yote muhimu. Mahitaji yanatofautiana toka chuo kimoja hadi kingine na kutegemeana na fani aliyoomba, na pia kama ni kutwa au bweni;

  6. Kwa utaratibu huu Mwombaji anaanza kujiunga na ngazi ya 1 (Level 1) ambayo ni ngazi ya chini. Waombaji wanaoendelea na ngazi za juu (Level II – III) vigezo ni ufaulu wa ngazi husuka unamwezesha kupanda ngazi nyingine.

Ada na Gharama za Mafunzo

Ada za mafunzo kwa kozi za muda mrefu kwa vyuo vinavyomilikiwa na VETA kwa sasa ni shilingi 60,000/= kwa mwanafunzi wa kutwa katika fani zote na bweni ni shilingi 120,000/=. Gharama zingine hutegemeana na fani na mahitaji mahsusi kwenye chuo husika.

Orodha ya vyuo na fani zinazotolewa kwenye vyuo husika zinapatikana kwenye tovuti ya VETA: www.veta.go.tz